Maonesho ya Ujasiriamali IAA Mwaka 2023

Mkurugenzi
wa masomo ya Astashahada, stashahada na shahada wa Chuo Cha Uhasibu Arusha
(IAA) Bi Gloria Kimburu ameipongeza idara ya usimamizi wa biashara (IAA) kwa
kuibua vipaji vya ujasiriamali kutokana na elimu wanayoitoa darasani kwa
wanafunzi na kuonesha kwa vitendo.
Bi
Gloria ameyasema hayo leo Februari 16, 2023 katika maonesho ya ujasiriamali (Entrepreneurship
Exhibitions) yaliyofanyika katika Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA), pia
amewashauri wanafunzi walioshiriki katika maonesho hayo kuwa na desturi ya
kujisomea vitabu mbalimbali ili kuongeza maarifa juu ya ujasiriamali.
Mkuu
wa idara ya usimamizi wa biashara Dkt. Martin Dome amesema kuwa kama idara
wanajivunia kuanzisha kozi ya usimamizi wa utaali na uanagenzi ambayo ndio
chanzo cha maonesho hayo.
Dkt.
Martin ameongeza kuwa ‘’tumeona umuhimu wa kuongeza baadhi ya lugha za kimataifa
tofauti na kiingereza kinachotumika sasa, katika Mtaala wa Usimamizi wa utalii
na uanagenzi hivyo tutakapokuwa tunafanya mapitio ya mtaala tutaona namna ya
kuongeza lugha hizo ili wanafunzi wetu waweze kuwafakia watu wengi duniani’’
Naye Bw.
Bakiri Angalia akiwasilisha mada amewaasa wanafunzi kuwa wabunifu kwa kuboresha
mawazo mbalimbali ya biashara na kutumia teknolojia iliyopo katika mazingira
yao ili kupunguza gharama za uendeshaji katika biashara zao.
Bw.
Elia Mbise mratibu wa maonesho hayo amesema; ’’Nimewafundisha namna ya kupata
wazo la biashara, kutambua fursa za biashara, namna ya kuandaa mipango ya biashara
na jinsi ya kutangaza biashara zao, lengo likiwa ni kuhakikisha kila mmoja
anakuwa na uwezo wa kufanya biashara na kushindana katika soko’’.
Mwita
mwagori mshiriki wa maonyesho ameuomba uongozi wa chuo kuwaunga mkono kwenye
biashara zao kwa kununua bidhaa wanazotengeneza pamoja na kuwawezesha katika
mawazo ya biashara waliyonayo; ili waweze kufika mbali kibiashara kwa kuwa
baadhi yao wamefanikiwa kufungua makampuni mbalimbali.
Maonesho
haya yamekuwa yakifanyika kila mwaka tangu mwaka 2019 ambapo mwaka huu
yameshirikisha wanafunzi wa mwaka wa pili wa shahada ya usimamizi wa utalii na
uanagenzi (Bachelor degree in tourism and hospitality management with
apprenticeship).